HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

18 November 2012

Rage kufikishwa mahakamani

Siku moja baada ya Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, kutangaza uamuzi wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo kulifuta tawi la Mpira Pesa pamoja na kuwafuta uanachama Mwenyekiti wa tawi hilo Masoud Awadh na Ally Bane, wanachama hao wamesema watalifikisha suala hilo mahakamani.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana kwa niaba ya Bane na yeye mwenyewe, Awadh alisema hawakubaliani na maamuzi ya uongozi wa Rage kuwafuta uanachama.
"Kwanza kauli ya Rage ya kusema kuwa sisi si wanachama halali si ya kweli kwa sababu mkutano mkuu wa mwisho wa klabu yetu tulihudhuria," alisema Awadh na kueleza zaidi:
"Sasa kwa nini alituruhusu kuhudhuria kwenye ule mkutano wakati anajua sisi si wanachama halali."
Alisema ni kwa msingi huo hakubaliani na maamuzi hayo ya Rage na kusema watahakikisha wanaipata haki yao hata kwa kulipeleka suala hilo mahakamani.
Aidha, alisema, bado wanatafuta sahihi za wanachama kwa ajili ya kuushinikiza uongozi kuitisha mkutano mkuu wa dharura wa klabu kujadili masuala mbalimbali ya Simba.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers