HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

22 December 2012

SIMUUZI KAKA NG'O!!! :Mourinho




Kocha wa Real Madrid  Jose Mourinho amesema hategemei kumuuza  Mshambuliaji wa timu hiyo Ricardo  Kaka Mwezi January .

MBrazil huyo ni moja kati ya wachezaji muhimu katika dimba la Bernabeu, lakini  Mourinho anataka kummbakiza mchezaji ili kuimarisha kikosi chake  .

Amesema : "Sidhani kama Kaka atakwenda popote  . atabaki hapa, na nimeshasema muda mrefu  ,kama akibaki ni vizuri kwanza anatungenezea mbinu mmbadala   ."

Mourinho alitumia nafasi hiyo kumtakia kocha wa  Barcelona  Tito Vilanova unafuu na kupona haraka vilanova mwenye Miaka  44-ameanza matibabu ya kupigana na ugonjwa  kansa .

Vilanova alifanyiwa upasuaji wa tezi ,ambapo klabu yake imesema ulifanikiwa kwa asimilia kubwa na sasa ataanza majuma sita ya mazoezi ya ya kulainisha misuli  .

"Kwa mambo kama haya huwa tunakuwa pamoja ,"aliongeza  Mourinho . "kwa  Tito,Na familia yake  na kwa yeyote mwenye tatizo la kiafya tunamtakia apate unafuu na apone ."

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers