HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

27 December 2012

Tunakabiliwa na tatizo kubwa


Kocha wa Manchester City, Roberto Mancini, amesema klabu hiyo inakabiliwa na tatizo kubwa kufuatia kushindwa kwa bao moja kwa bila na Sunderland.

Mabingwa hao watetezi, walipoteza nafasi nyingi za kufunga wakati wa mechi hiyo, na kupoteza alama tatu muhimu, hatua inayowaweka alama saba nyumba ya vinara wa sasa Manchester United.

Man City imefunga magoli 34 baada ya kucheza mechi 19, katika mechi za ligi kuu msimu huu, idadi ambayo ni magoli kumi na nne chini ya magoli waliyofunga mahasimu wao Manchester United ambao waliilaza Newcastle 4-3 siku ya Jumatano.

Zaidi ya yote Man City imefunga magoli 12 kwa mechi tisa za ugenini ukilinganisha na United ambayo imefunga magoli 22 kutoka kwa mechi 10.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers