HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

25 January 2013

SERIKALI YAFYATA ,MKIA KUCHUKUA %15 TU YA MAPATO YA UWANJA WA TAIFA MAKUBALIANO YAFIKIWA BAINA YAO, TFF NA BODI YA LIGI.


 

Hatimaye Serikali imekubali kupunguza kiasi cha makato ya mapato ya michezo inayochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam na sasa itakuwa ikichukua asimilia 15 tu ya mapato ya michezo yote itakayokuwa ikichezwa katika uwanja huo.
Hayo yamo ndani ya makubaliano yaliyofikiwa baina ya pande tatu yaani serikali, shirikisho la soka nchini TFF na bodi ya ligi makubaliano ambayo yamesainiwa baada ya kikao cha wiki iliyopita.
Hii leo katika ofisi za wizara ya habari, utamaduni na michezo huku serikali ikiwakilishwa na naibu waziri Amos Makala na mkurugenzi wa michezo Juliana Yasoda nayo TFF ikiwakilishwa na katibu mkiuu wake Angetile Oseah na bodi ya ligi ambayo bado haijaundwa ikiwakilishwa na afisa mtendaji mkuu wake Silas Mwakibinga yamesainiwa makubaloiano hayo.
Makubaliano hayo sasa yatakuwa yanaleta unafuu kwa vilabu na timu za taifa ambazo mara kwa mara zimekuwa zikiuutumia uwanja huo katika michezo ya ligi na michuano ya kimataifa kwa ngazi mbalimbali.
Hata hivyo bado maumivu ya makato ya uwanja huo yanaonekana kama yataendelea kwa namna moja ama nyingine kwa kuwa bado kuna makato mengine hayajapata nafuu yake kwa kuwa bado yatakuwa yakiendelea kama vile makato ya gharaza za mchezo, maandalizi ya mechi, mashine za uwanjani , umeme na usafi pamoja na ulinzi bila kusahau chama cha soka mkoa mwenyeji wa uwanja Dar es Salaam DRFA.
Akiongea mbaele ya waandishi wa habari naibu waziri wa habari Amos Makalla amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya kuwepo kilio cha muda mrefu na kwa kuwa serikali ni sikivu imeamua kuchukua hatua hiyo muhimu kwa kushirikiana na TFF na bodi ya ligi.
Kuhusu suala la malipo ya fedha za makocha ambazo zimepelekea akaunti ya TFF kuzuiliwa na mamlaka ya mapato nchiniTRA, Makalaa amesema suala hilo linashughulikiwa na kwamba linakwenda vizuri likiwa katika hatua za mwisho mwisho na kwamba kinacho subiriwa ni malipo ya kurudisha fedha hizo kwenye akaunti iliyofilisiwa.
Pia amesema kwamba serikali itajitahidi jambo hilo lisijirudie tena.
Pia Makalla amevipongeza vilabu vinavyoshiriki ligi kuu kwa kukubali kuingia katika mzunguko wa pili wa ligi kuu unaoanza hapo kesho licha ya kwamba vinakabiliwa na mazingira magumu ya kutokuwa na fedha ambazo zimefungiwa katika akaunti hiyo ambayo ni maalumu kutunza fedha za vilabu zinazotoka kwa mdhamini wa ligi kampuni ya Vodacom.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers