Timu ya Young Africans Sports  Club kesho itashuka dimbani kucheza 
na timu ya Denizlispor FC ya ligi daraja la kwanza nchini Uturuki katika
 mchezo wa kirafiki utakaofanyika katika uwanja wa Selen Football 
-Kalimya Complex pembeni kidogo ya mji wa Antlaya.
Young Africans ambayo imeweka kambi ya mafunzo 
jijini Antalya itatumia mchezo huo kama fursa ya kujipima nguvu na timu 
hiyo la Denizlispor FC  ambayo imeshuka kutoka ligi kuu ya Uturuki mwaka
 jana na hivi sasa inapamabana kurudi tena katika Ligi Kuu ya Uturuki.
Kocha
 Mkuu wa Young Africans Ernest Brandts amesema kwao ni furaha kupata 
nafasi ya kucheza na timu kubwa kama ya Denizlispor FC ambayo ina 
wachezaji wa kiwango cha kimataifa hivyo anaamini utakua ni mchezo safi 
na kuwavutia.
Baada ya kuwa na 
wiki moja ya mazoezi na mechi moja ya kirafiki dhidi ya Armini Bielefeld
 ya ujerumani mwishoni mwa wiki itakua ni fursa nyingine nzuri ya 
kucheza mchezo wa kirafiki na timu nyingine, hii itanisadia kuona 
maendeleo ya kikosi changu kutokana na mazoezi ambayo tumekuwa 
tukiyafanya tangu tulipofika alisema 'Brandts'
Denizlispor
 FC ni miongoni mwa timu zaidi ya 200 kutoka shemu tofauti duniani 
ambazo zimeweka kambi katika mji wa Antlaya kwa ajili ya maandilizi ya 
mzunguko wa pili wa Ligi Daraja la kwanza nchini Uturuki.
Mchezaji
 wa zamani wa Leicester City ya Uingereza, Dundee United ya Scotland na 
Ivernes ya Uholanzi, mtanzania mzaliwa wa Uingereza Eric Odhiambo ni 
miongoni mwa washambuliaji wa kutegemewa wa timu ya Denizlispor FC. 
Young Africans imeendelea na mazoezi katika viwanja wa Fame 
Residecne tayari kabisa kujiandaa na mchezo huo utakaochezwa kesho 
katika uwanja wa Selen Football - Kalimya complex pemebeni kidogo ya mji
 wa Antalya.
Kikosi cha wachezaji 27 waliopo 
mjini Antalya wote wako katika hali nzuri na hakuna maheruhi hata mmoja 
hali itakayompa kocha Brandts kuamua kumtumia mchezaji yoyote katika 
mchezo huo.
Athumani Idd 'Chuji' na Hamis Kiiza 
waliokuwa wakijisikia vibaya kabla ya mchezo wa juzi dhidi ya Amrnini 
Bielefeld wanaendelea vizrui kabisa kwani wanaendelea na mazoezi pamoja 
na wachezaji wengine waliopo na timu mjini Antalya. 
Kuhusu
 hali ya hewa leo haijaonekana kuwa tatizo kwa wachezaji kwani 
wanaonekana kuimudu na mda mwingi kwa sasa kumekua na jua linalowaka 
kuanzia asubuhu wakati wa mazoezi mpaka mida ya jioni, kwa leo hali ya 
hewa ni nyuzi joto 17 - 21, hivyo hali ya hewa ni nzuri kabisa na jua 
linawaka mda wote.
 
 
 
No comments:
Post a Comment