HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

19 December 2012

ZFA IPO SAHIHI ADHABU SI SAHIHI



Chama soka cha Zanzibar ZFA wiki hii kiliwafungia wachezaji waliohusika kugawana fedha za ushindi wa tatu katika mashindano ya Cecafa yaliyofanyika  huko Uganda na wenyeji kutwaa Ubingwa .


 katika hari isiyoyakutegemewa chama hicho kimewafungiwa Nadir Haroub Ali " Cannavaro, msaidizi wake Agrey Morris, Khamis Mcha " Viali" Nassor Masoud " " Cholo" Twaha Mohammed, Suleiman Kassim " Serembe" na Abdallah Seif kwa kosa la kugawana fedha hizo wakiwa nchini Uganda Chama hicho kimewafungia Mwaka mmoja wachezaji huku kikilitaka shirikisho la soka la Tanzania kutambua adhabu hiyo jambo ambalo wadau wengi wametokea kulipinga na wengine kuliafiki K-SPORT.COM imeamua kukusanya baadhi ya Data na kulitazama jambo kwa pande mbili za sarafu .



Upande wa kwanza ingekuwaje kama kitendo hiki kingefanywa na wachezaji wa Tanzania bara Je tff ingeridhia na kukiona cha kawaida ? jibu la haraka sio kweli hata  kidogo Tanzania iliwahi kucheza na Cameron na Nadir Ali alibadilishana jezi na Samuel Eto’o jambo lililozua gumzo nchini kiasi kufikia baadhi ya wadau kulipa fedha hizo taslimu  baada ya shirikisho kumtaka arejeshe jezi pengine mungu alitaka kumtumia Nadir haroub kuonyesha kuwa wachezaji wetu hurudia jezi moja au wanapea moja ya jezi kwa  mechi zote  .


Tuonavyo ilikuwa ni jambo la TFF na ZFA kukaa  pamoja na kujadiri swala hili na sio kila upande kufanya wachofikiri ni sahihi – kwa upande mwingine ZFA ina  haki kwani ni  kitendo  cha kuidharirisha taifa hili dogo lisilofahamika katika soka ya kimataifa lakini likifahamika katika Ukanda  wa afrika mashariki na kati huku likiwa mwanachanma wa muda wa shirikisho la soka barani afrika CAF .


Yamkini ZFA walichotakiwa kufanya ni kutazama aina ya adhabu kwani katika ulimwengu wa leo huezi kumfungia mchezaji mwaka mzima kwa kosa la kugawana fedha wakati adhabu hiyo mara nyingi hutolewa kwa makosa ya rushwa au kupanga matokeo hakika kwa hili ZFA inayohaki haki kuwaadabisha wachezaji lakini sio kwa kiasi cha adhabu walichopewa  ni adhabu kubwa kuliko mategemeo lakini  kubwa zaid TFF inatakiwa kukaa chini na kukemea swala hili sio swala la ZFA pekee kwani-; 

 leo inaonekana kama Zanzibar Heroes haipewi heshima hata kidogo kwani  si jambo jema K-SPORT inazishauri ZFA kutumia hekima na kukaa chini na TFF kuheshimiana na kujadiliana katika  stahiki na nidhamu ya vyama husika na kuwa na nidhamu katika kuheshimiana na wachezaji wawe na nidhamu kutii na kuwajibika inavyotakiwa .


ZFA NA TFF KAENI CHINI PAMOJA NIDHANU LAZIMA IZINGATIWE

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers