Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF) limemtangaza Albert
Sokaitis kutoka Marekani kama mkufunzi wa kunoa makocha wa mchezo huo
nchini na timu ya taifa ya kikapu huku mkufunzi huyo akisema kuwa lengo
lake kuu ni kusaka vipaji vya mchezo huo wenye wapenzi wengi nchini
kwao.
Rais wa TBF, Musa Mziya amesema kuwa mkufunzi huyo ataanza kwa kutoa mafunzo katika kanda ya Dar es Salaam wakati akiangalia mazingira kabla ya kuingia nao mkataba, ambao wanafikiri kuwa wa miaka miwili.
Akifafanua kuhusu mipango yake, Sokiatis amesema kuwa atakuwa na jukumu la kufundisha makocha na kusaka vipaji vya mchezo huo huku akiwatafutia wachezaji nafasi za kuonyesha vipaji vyao nje ya mipaka ya Tanzania.
Rais wa TBF, Musa Mziya amesema kuwa mkufunzi huyo ataanza kwa kutoa mafunzo katika kanda ya Dar es Salaam wakati akiangalia mazingira kabla ya kuingia nao mkataba, ambao wanafikiri kuwa wa miaka miwili.
Akifafanua kuhusu mipango yake, Sokiatis amesema kuwa atakuwa na jukumu la kufundisha makocha na kusaka vipaji vya mchezo huo huku akiwatafutia wachezaji nafasi za kuonyesha vipaji vyao nje ya mipaka ya Tanzania.
No comments:
Post a Comment