Chama cha mchezo wa netiboli nchini (CHANETA) kinatarajia kukutana Mei
31 kwa ajili ya kujadili uteuzi wa kocha mkuu wa timu ya taifa ya
netiboli inayojiandaa kushiriki mashindano ya ubingwa wa Afrika.
Mashindano hayo yanayoshirikisha timu za taifa kutoka nchi mbalimbali za Afrika yamepangwa kufanyika Juni mwaka huu nchini Malawi.
Mwenyekiti wa CHANETA, Anna Kibira amesema Taifa Queens inahitaji kocha mpya kwa sababu kocha Mary Waya amemaliza mkataba wa kuinoa timu hiyo tangu mwaka jana.
Kibira amesema jambo hilo linawalazimisha kukutana kutafuta kocha mpya.
"makocha wapo wengi lakini lazima viongozi wote wakutane na kujadili nani anayesteahili kupewa timu hiyo".
Wakati huo huo, CHANETA inatarajia kukutana na chama cha netiboli cha Zanzibar (CHANEZA) kwa ajili ya viongozi kufahamiana ikiwamo kupanga mikakati ya kuendeleza mchezo wa netiboli nchini. kikao cha pamoja kinatarajia kufanyika Juni Mosi mjini Zanzibar, ambapo wajumbe wote watahudhuri na kupeana mikakati ya kuinua mchezo wa netiboli.
"Tunatarajia kwenda Zanzibar kukutana na viongozi wa kule, lengo ni kudumisha umoja wetu kwa manufaa ya mchezo huu," alisema Kibira.
Vyama hivyo vimekuwa vikivutana kwa miaka mingi.
Mashindano hayo yanayoshirikisha timu za taifa kutoka nchi mbalimbali za Afrika yamepangwa kufanyika Juni mwaka huu nchini Malawi.
Mwenyekiti wa CHANETA, Anna Kibira amesema Taifa Queens inahitaji kocha mpya kwa sababu kocha Mary Waya amemaliza mkataba wa kuinoa timu hiyo tangu mwaka jana.
Kibira amesema jambo hilo linawalazimisha kukutana kutafuta kocha mpya.
"makocha wapo wengi lakini lazima viongozi wote wakutane na kujadili nani anayesteahili kupewa timu hiyo".
Wakati huo huo, CHANETA inatarajia kukutana na chama cha netiboli cha Zanzibar (CHANEZA) kwa ajili ya viongozi kufahamiana ikiwamo kupanga mikakati ya kuendeleza mchezo wa netiboli nchini. kikao cha pamoja kinatarajia kufanyika Juni Mosi mjini Zanzibar, ambapo wajumbe wote watahudhuri na kupeana mikakati ya kuinua mchezo wa netiboli.
"Tunatarajia kwenda Zanzibar kukutana na viongozi wa kule, lengo ni kudumisha umoja wetu kwa manufaa ya mchezo huu," alisema Kibira.
Vyama hivyo vimekuwa vikivutana kwa miaka mingi.
No comments:
Post a Comment