Mchezaji wa timu ya soka ya AC Milan Mario
Balotelli amekumbana na kadhia ya ubaguzi wa rangi kutoka kwa mashabiki na kusababisha mwamuzi Gianluca Rocchi kusimsmisha mtanganae huo katika kipindi cha pili baada ya kusimama kwa dakika kadhaa katika kipindi hicho ilibidi watangaze kiwanjani kuipinga tabia hiyo mchezo huo ulikwisha kwa timu hizo kwenda suluhu ya kutokufungana .
Kocha wa AC Milan Massimiliano Allegri alisema baada ya mechi hiyo kuwa maamuzi ya maafisa kuisimamisha mechi bado hayakutosheleza ilibidi kuchukuliwa hatua zaidi .
"katika maoni yangu ,kuna suluhisho moja tu la kufanya inapotokea swala la ubaguzi ni kuvunja mechi ," Allegri amezungumza hayo katika tovuti ya klabu hiyo .
"kuonyesha msisitizo kwa tatizo hili ni kutoa mamuzi makubwa zaidi . tunaweza kuadhibu watu siku za usoni na itatusaidia kama taifa siku zijazo na kuonyesha uungwana .
No comments:
Post a Comment