Timu ya soka ya Taifa ya Tanzania
Imelazimshwa sare ya mabao mawili kwa mawili Dhidi ya Msumbiji katika
mchezo wa kuwania kufuzu Mataifa ya Afrika yatakayofanyika Nchini
Morocco mwakani .
ilichukua Dakika moja tu tangu kuanza
kwa kipindi cha pili kwa msumbiji kuliona Lango Tanzania kwa Mkwaju wa
Penati baada Kelvin Yondani Kumfanyia Faulo mshambuliaji wa Msumbiji na
mwamuzi kuamuru ipigwe Penati.
Stars walipigana kufa na kupona mpaka
pale alipoingia Hamis Mcha katika dakika ya sitini badala mrisho Ngasa
na kusawazisha Goli hilo kwa mkwaju mkali , Voley kutoka upande
mashariki wa kiwanja na kumwacha Mlinda mlango wa msumbiji Ricado Campos
asijue cha Kufanya .
Dakika tano Baadae Beki wa timu ya
Msubiji alimfanyia Faulo Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania
anayechezea klabu ya Tout Puisant Mazembe ya Congo na kumwachia Jukumu
kijana wa Kizanzibar Hamis ncha kufunga Bao la Pili .
Stars iliendelea kulisakama lango la
msumbiji na alimanusula ipate bao la tatu pale mpira uliopigwa na samata
kugonga mlingoti wa Goli lakini Baadae mlinga Mlango wa msumbuji
aliudaka na kuanzisha Kaunta Ataki na kuipatia msumbji goli la
kusawazisha lilofungwa na Isaac Calvaho akipokea pasi kutoka kwa Domingues baada ya Yondani kupigwa kanzu na kuipatia Sare timu yake .
Timu hizo zitarejeana baada ya majuma mawili Huko maputo nchini Msumbiji.
PICHA BIN ZUBERY
No comments:
Post a Comment