HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

7 September 2012

MECHI YA NGAO YA JAMII KUCHANGIA HOSPITALI YA TEMEKE


Picha na Kandanda
Asilimia tano ya mapato yatakayopatikana kwenye mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kati ya Simba na Azam yatakwenda kwenye Hospitali ya Temeke mkoani Dar es Salaam.
 
Kabla ya kukabidhi, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litakutana na uongozi wa Hospitali ya Temeke kupanga maeneo ambayo fedha hizo zitatumika kwenye hospitali hiyo.
 
Mechi hiyo ya uzinduzi rasmi wa msimu wa 2012/2013 itafanyika Jumanne ya Septemba 11 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
 
Viingilio kwenye mchezo huo vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa viti vya VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers