HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

13 September 2012

SIMBA YAHAMIA POLISI DHIDI YA KELVIN YONDAN



Kamati ya utendaji ya mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara klabu ya Simba imekubali kuirejesha katika ligi kuu ya Tanzania Bara timu yao baada ya kikao cha kamati hiyo kukutana na kujadili taarifa ya kamati ya maadili nidhamu na hadhi ya wachezaji ya Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF chini ya mwenyekiti wake Alex Mgongolwa.
SIKIZA HAPA   
 
Kamati hiyo iliwahalalisha wachezaji Yondani na Twite kuchezea Yanga ambao ni mabingwa wa kombe la Kagame kwa mujibu wa kanuni za TFF na  FIFA jambo ambalo lilipelekea klabu ya Simba kutishia kujitoa katika ligi kuu na michuano yote inayoandaliwa na TFF.
Pia kamati hiyo ya Utendaji imewataka wanachama wa klabu hiyo waliokuwa wamejipanga kwenda mahakamani kuishitaki TFF kuacha kufanya hivyo kwani klabu hiyo imeamua kusonga mbele zaidi kwa kuupeleka mkataba wa Yondani Polisi kupata ukweli kuhusu saini ya kidole gumba cha mchezaji huyo na kutoa majibu ya kama alisaini Simba ama lah.
SIKIZA HAPA
 
ROCKER SPORTS UNDSTAND

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers