HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

23 November 2012

Mark Huges KAMA DI MATEO JE NANI ATAWAFUATA ?

Mark Hughes 

Kocha wa QPR, ambayo kwa sasa iko mkiani kwenye msimamo  wa ligi kuu ya Premier ya Uingereza  Mark Hughes amefukuzwa  kazi.
Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwa bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo,
 kocha huyo amefukuzwa kazi kutokana na matokeo mabaya tangu kuanza kwa msimu huu.

Baada ya mechi 12 kuchezwa QPR haijashinda hata mechi moja.
Taarifa hiyo imesema kuwa, bodi hiyo inajadili mipango ya kutangaza wasimamizi wapya wa klabu hiyo muda mfupi ujao.
Mark Bowen na Eddie Niedzwiecki watasimamia klabu hiyo wakati wa mechi ya ya kesho Jumamosi dhidi ya Manchester United katika uwanja wa Old Trafford.

''Bodi ya wakurugenzi ingependa kutoa shukrani kwa Mark, kutokana na juhudi zake wakati akiwa kocha wa klabu hiyo kwa muda wa miezi kumi iliyopita'' taarifa hiyo iliongeza.
Wakurugenzi hao wamesema watatangaza mipango mipya ya klabu hiyo muda mfupi ujao na aliyekuwa kocha wa Tottenham Harry Redknapp anatarajiwa na wengi kuteuliwa kuwa kocha mpya wa QPR.


No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers