
 WAOMBAJI
 uongozi kuwania nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Shirikisho la 
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board) waliokata 
rufani kupinga kuenguliwa kwenye kinyang’anyiro hicho wanaruhusiwa kuwa 
na uwakilishi wa kisheria (legal representation) wakati wa kusikilizwa 
rufani zao.
Uamuzi
 wa kuruhusu mawakili kwenye usikilizaji wa rufani hizo mbele ya Kamati 
ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF inayoongozwa na Idd Mtiginjola ni 
kuhakikisha kila upande unapata haki.
Pia
 Kamati ya Uchaguzi ya TFF ambayo ndiyo iliyosaili waombaji uongozi, 
hivyo kuwa mlalamikiwa katika rufani hizo, nayo inaruhusiwa kuwa na 
Wakili wakati wa usikilizaji wa rufani hizo.
Kamati
 ya Uchaguzi ya TFF iliwaengua waombaji kumi na mbili wa uongozi kwenye 
nafasi mbalimbali katika uchaguzi huo utakaofanyika Februari 24 mwaka 
huu jijini Dar es Salaam kwa kutokidhi matakwa ya kikatiba. Uchaguzi wa 
TPL Board utafanyika Februari 22 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Waombaji
 hao waliochujwa ni Omari Mussa Nkwarulo aliyeomba kuwania urais na 
Michael Richard Wambura aliyejitosa katika kinyang’anyiro cha nafasi ya 
Makamu wa Rais. 
Wengine
 waliochujwa wakiomba kugombea nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni
 Abdallah Hussein Musa, Mbasha Matutu, Charles Mugondo, Ayubu Nyaulingo,
 Nazarius Kilungeja, Eliud Peter Mvella, Farid Nahdi, Omari Isack 
Abdulkadir na Shafii Kajuna Dauda.
Kwa
 upande wa uchaguzi wa Bodi ya Ligi Kuu aliyechujwa ni Christopher Peter
 Lunkombe aliyekuwa akiomba nafasi ya ujumbe katika Kamati ya 
Uendeshaji.
Mwisho
 wa kukata rufani kwa waombaji uongozi walioenguliwa na wale walioweka 
pingamizi kwa wagombea na zikatupwa ni leo (Februari 7 mwaka huu) saa 10
 kamili jioni. 
No comments:
Post a Comment