Pambano
 la kirafiki la kimataifa kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Cameroon 
(Indomitable Lions) lililochezwa jana (Februari 6 mwaka huu) na wenyeji 
Stars kuibuka na ushindi wa bao 1-0 limeingiza sh. 148,144,000.
Fedha
 hizo zimepatikana kutokana na watazamaji 23,092 waliokata tiketi 
kushuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 
10,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
Mgawanyo
 wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko 
la Thamani (VAT) ni sh. 22,598,237.29, maandalizi ya mchezo sh. 
58,000,000 wakati wa gharama za uchapaji tiketi ni sh. 7,340,900.
Nyingine
 ni bonasi kwa wachezaji wa Taifa Stars sh. 18,831,864.41, asilimia 20 
ya gharama za mchezo sh. 8,274,659.66, asilimia 15 ya uwanja sh. 
6,205,994.75 na asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) 
sh. 2,068,664.92.
Asilimia
 60 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 24,823,978.98 na 
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,241,199 
ambayo ni asilimia 5 kutoka kwenye mgawo wa TFF.
No comments:
Post a Comment